WE ARE UNDER CONSTRUCTION........COMING BACK SOON
Most Popular

Jumapili, 3 Julai 2016

Rais John Pombe Magufuli awatega wakuu wa wilaya 20

Baada ya Rais John Magufuli kufanya uteuzi wa wakuu wa wilaya 139, homa sasa imehamia kwa wakuu wa wilaya 20 ambazo zinakabiliwa na changamoto kubwa kutokana na kukabiliwa na migogoro mingi ikiwamo matatizo ya maji, njaa na mapigano ya wakulima na wafugaji.

Changamoto inayowafanya wakuu hao kukalia kuti kavu iwapo watashindwa kupambana kikamilifu na changamoto hizo inatokana na vigezo vilivyowekwa na Rais Magufuli ambavyo alivitumia wakati wa kuwateua ambavyo ni migogoro ya ardhi, tatizo la elimu hasa upungufu wa madawati, njaa na mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu.

Wakuu wapya ambao wanakabiliwa na mtihani huo ni pamoja na Mohamed Utali (Mvomero), Adam Mgoyi (Kilosa), Luteni Kanali Michael Mtenjele (Ngara), Rashid Taka (Ngorongoro), John Palingo (Kongwa), Tumaini Magessa (Kiteto), Josephat Maganga (Bukombe), Thobias Mwilapwa (Tanga), Glodius Luoga (Tarime), Asia Abdallah (Kilolo) na Godwin Gondwe (Handeni).