WE ARE UNDER CONSTRUCTION........COMING BACK SOON
Most Popular

Jumamosi, 25 Juni 2016

Kamati ya Bunge ya Katiba na Sheria ya mgomea Rais Magufuli katika kuanzisha mahakama ya mafisadi

Kamati ya Bunge ya Katiba na Sheria imepinga pendekezo la Rais kushauriana na Jaji Mkuu katika kuanzisha Mahakama ya Ufisadi na Uhujumu Uchumi, ikieleza kuwa hatua hiyo ni kuingilia mhimili wa Mahakama.

Mwenyekiti wa kamati hiyo, Mohamed Mchengerwa licha ya kupongeza hatua ya Serikali kuanzisha divisheni hiyo alisema kamati yake haioni mantiki ya Rais kuingilia mamlaka ya Jaji Mkuu katika kuanzisha mahakama hiyo.

Katika marekebisho ya Sheria ya Usimamiaji Haki na Matumizi ya Sheria, Sura 358 yaliyowasilishwa bungeni na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, George Masaju, kifungu kipya 4A kinamwezesha Jaji Mkuu kuanzisha mahakama hiyo lakini kwa kushauriana na Rais.